- Kampuni ya umeme humu nchini ya Kenya Power imekiri kuwa imekuwa ikiwatoza wateja wake zaidi
- Kulingana na kampuni hiyo, gharama kubwa ya mafuta ndiyo sababu ya ongezeko la bili za stima
Kampuni ya usambazaji stima humu nchini, Kenya Power imewaomba Wakenya radhi kufuatia ongezeko la bei ya stima, tatizo kuu ambalo limeangaziwa hivi karibuni na Wakenya.
Habari Nyingine: Lilian Muli hatimaye azungumzia uvumi kuwa alipachikwa mimba na Jeff Koinange
Kenya Power imekiri kuwa imekuwa ikiwatoza Wakenya zaidi kwa kipindi cha miezi minne.
Hatua ya Kenya Power inajiri siku chache tu baada ya kuwaomba Wakenya na hasa viongozi wa kisiasa kusameheana siku ya Jumatano, Mei 2.
Habari Nyingine: William Kabogo ajipata pabaya baada ya kumtumia 'slay queen' ujumbe
Hapo awali, waziri wa Kawi, Charles Keter alipinga vikali kuwa kampuni hiyo ambayo ndiyo pekee iliyojukumiwa kusambaza stima nchini imekuwa ikiwatoza Wakenya zaidi kuliko inavyostahili.
Kulingana na kampuni hiyo, zaidi ya 82% hutumika kulipia gharama za kampuni hiyo kuliko vipimo vyenyewe vya stima, kumaanisha Kenya Power hupata faida kidogo tu kutokana na vitu vingi ambavyo hulipia.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Habari Nyingine: Vera Sidika arekodi video ya shabiki wake wa kiume aliyemuacha hoi, amuahidi zawadi
Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Ken Tarus aliahidi kuwa bili itapungua kwani kiwango cha maji katika mabwawa kimeongezeka kutokana na mvua kubwa.
"Tumeshuhudia ongezeko la maji katika mabwawa makuu. Hii ina maana kuwa gharama ya mafuta itapungua," Alisema Tarus.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibH96fpdmq66mkaS6o62MpqqapZGdrm63xKewmmWgpMSmvoyymLCZn6KvonnWmqKepqmWeq6%2FwKaYoZmblnqsw8Bmoq6vkam8u62Ms5iinJliuKLAyKSYZqOlobaxtcBmqq2hnZZ7qcDMpQ%3D%3D