Watu 7 wakamatwa wakijaribu kuingia Kaunti ya Kirinyaga kisiri
-Maswali yameibuliwa ya namna wasafiri saba walifaulu kupita vizuizi vyote vya kaunti za Nairobi, Kiambu na Murang'a
- Washukiwa hao walijaribu kuwahonga polisi katika eneo la Kutus, Kirinyaga kabla ya kukamatwa na kupelekwa karantini
- Sita kati yao ni wa asili ya Somali huku mmoja akiwa ni Mkenya walisafirishwa hadi Karen, Nairobi kwa karantini ya siku 14
Watu saba wamekamatwa baada ya kuingia katika kaunti ya Kirinyaga wakiwa safarini kuelekea Garissa kutoka Nairobi.